Sala kwa ajili ya Jubilei ya miaka 25 tangu
ilipoanza Misioni yetu ya Tanzania
Ee, Mungu, Bwana na Baba yetu tunakushukuru kwa kazi ya mikono yako,
kila kitu tunachokiona ni tuzo kutoka kwako, zawadi ya Maongozi yako.
Tunakushukuru kwa ajili ya wale wote ambao wameshiriki katika ukuaji wa Misioni hii.
Kila siku Wewe umetutangulia katika kila kazi na kwa upendo wako umefanya Misioni yetu iwe bustani nzuri sana, machoni pa watu wengi.
Sisi sote tunakushukuru!
Yote uliyotuahidi umeyatimiza kwa nguvu ya uwepo wako, na ya Upendo wako wa kibaba.
Sisi sote tunakushukuru!
Uangalizi wako wa Baba mwenye upendo umeimarisha nguvu zetu na ari yetu ya kukutumikia
Sisi sote tunakushukuru!
Wewe unaendelea kuiangalia na kuitegemeza kwa njia ya Roho wako Misioni yetu kwa sababu uliijenga kwa ajili yako mwenyewe kama sehemu ya baraka
Sisi sote tunakushukuru!
Bwana, kila kitu ni zawadi yako, hatuna chochote cha kukurudishia isipokuwa makosa yetu na udhaifu wetu. Tunakuomba msamaha Bwana, kwa sababu hatujakurudishia chochote kinacholingana na upendo wako mkubwa na neema zako nyingi. Ee Bwana usiiache kazi ya mikono yako! Endelea kulibariki Shirika letu na Misioni yetu kwa kutupatia miito mingi na mitakatifu na pia endelea kutusaidia kutimiza kwa uaminifu ahadi tulizokuwekea. Tunakuomba si kwa mastahili yetu, kwa sababu hatustahili, bali kwa mastahili ya Kristo Yesu Mwanao. Kwa maombezi ya Bikira Maria Bibi wa Misioni yetu, ya Mtakatifu Yosepu mhasibu wetu, mt. Ursula, fanya ili sisi sote tuisikie leo nguvu ya enzi yako, ya utukufu wako juu ya Misioni yetu na juu ya kila mursula wa Tanzania. AMINA