Mursula kwa wito wake anajiunganisha kwa namna ya pekee na Fumbo la Mateso ya Kristo ambaye akitumwa na Baba, aliwapenda hivyo wanadamu hata kujitoa mwenyewe kama sadaka kwa njia ya kifo chake msalabani. Kwa njia ya mateso yake wanadamu wote washiriki kifo chake na ufufuko wake, ili waufikie uzima wa milele. Masista wanajaribu kuitikia neno la Kristu: “Ninaona kiu” wakijitolea mhanga kikamilifu kwa upendo wa Moyo wa Yesu, pasipo kiasi, wakishirikiana kwa ajili ya wokovu wa wanadamu.
Kielelezo cha maisha ya masista waursula ni maneno ya Bikira Maria aliyomjibu malaika: „Tazama mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena” . Maneno haya ni „motto” wa waursula wa Moyo Mtakatifu wa Yesu Mteswa